Showing posts with label sun. Show all posts
Showing posts with label sun. Show all posts

Saturday, August 27, 2011

Zawadi sehemu ya tatu...


Sehemu ya tatu...

Alinishika mkono wa kulia kwa nguvu na kunivuta ulipokua mlango wa chumbani. Bila kunitazama usoni aliuachia mkono wangu na kunisukuma kitandani , hapo ndipo akili yangu iliporudi. Nilijua nini alichokusudia kufanya na nilihitaji namna ya kuzuia kitendo kile.Kwa haraka niliinuka toka kitandani ili nitoke mbio ila sikupata mwanya huo maana mara hii baada ya kunisukumu alinikandamiza chini kwa mikono yote miwili. Mpaka wakati huo bado sikuelewa mabadiliko yale yalitokana na nini haswa. Macho yake yaliyokua yakinivutia mwanzoni yalinitazama kwa ukali, na kwa mara ya kwanza niliogopa kuangaliwa nayo.
“ Unaniumizaaa“ nililia kwa sauti ya chini. Hakuonekana kujali kwani ndio kwanza alinitazama kwa ukatili. “Malaya mkubwa wewe.“ alisema kwa gadhabu, “Huna shukurani kabisa. Unakula pesa yangu kumbe unaliwa na wengine huko?! Ngoja nikufundishe heshima kidogo“ alisema huku akiwa ameshika shati langu tayari kulirarua.

Machozi yalinitiritika sambamba na sauti ya vifungo vilivyoanguka sakafuni, vilivyogonga ukutani na pia sehemu ya kitanda.Alisogeza uso wake kifuani kwangu kama mtu anaechunguza kitu kisha akaupandisha taratibu.Midomo yake ilipokaribia yakwangu nikafikiria namna ya kumuondoa juu yangu, alipoikutanisha tu yangu na yake nilimng‘ata japo sio kiasi cha kumtoa damu!! “Mamaaa“ alilia huku akiruka kwa maumivu na kujilaza chali pembeni yangu huku akichunguza midomo yake kwa ulimi na mkono wake.Nikatumia mwanya ule kukimbia mpaka sebuleni na moja kwa moja nilielekea mlangoni.Mkono wangu ukiwa umeshika kitasa cha mlango tayari kuufungua nilihisi maumivu makali shingoni. Alinigeuza akanitazama kwa hasira kisha akanikokota tena mpaka lilipokuwapo sofa bila kusema neno. Alinisukuma kisha akanyanyua miguu yangu na kuiweka juu. “Sasa urudie tena ushenzi uliofanya uone ntakachokufanya.Hivi wewe unanijua au unanifahamu?!“ ......“Si nakuuliza wewe?!“ alinizodoa kwa kidole. Sikuweza kujibu maana kilio na kwikwi vilinitawala.

Thursday, August 25, 2011

Dondoo za mapenzi...



Mahsusi kwa watu wanaotarajia kuanzisha mahusiano thabiti na yenye malengo pamoja na wale ambao tayari wamo ndani ya mahusiano ya aina hiyo.

KWA WATARAJIA

1.Usidanganyike na muonekano wa nje au yale maongezi ya mwanzo.
Kila mtu hua mstaarabu siku za mwanzo hata wale ambao sio.

2.Usikimbilie kutangaza nia haraka.
Siku zote ni rahisi mtu kua muwazi kwa rafiki yake kuliko kwa mtu ambae anajua anataka mahusiano nae kwa hofu ya kumpoteza.Tumieni muda wakutosha kufahamiana kama marafiki kabla hamjajiingiza kwenye uhusiano wa kimapenzi.

3.Uliza maswali kuhusu vitu ambavyo ni muhimu sana kwako.
Kwa mfano kama ni mtu wa familia au sio taka kujua mawazo yake kuhusu watoto hii itaepusha migongano isiyo ya lazima hapo baadae.

4.Penda kujua malengo yake ya baadae.
Hii itakuwezesha kugundua ni mtu wa aina gani...kama ni mpenda maendeleo,mtu wa starehe tu n.k.

5.Kua muwazi.
Hii inakwenda kwa pande zote...kuna vitu ambavyo ukimwambia mtu ni vidogo sana ila ukificha vinakua kwa vile tu ulifanya siri.

6.Hakikisha uwezo wenu wa kuelewa unaendana.
Hapa siongelei darasa ila mnavyokua sambamba kwenye maongezi ya kawaida tu yasiyo hitaji degree.

Once a stranger....


Once a stranger...




You were once a stranger...
a man with character...
but yet could not be read like a blank piece of paper.

I asked for your name and you did the same...
was that fate?! I think not...
just a connection we had to create!

The tone of your voice like music to my ears...
the depth of your story brought me close to tears!
Ohhh what a lovely man....
with a bright personality much like the sun!

I wished to stare into your eyes...
to feel what they disguised!
See if you told lies ..and whether you were wise!
What I learned...was more than I had earned!

Now months later..you are no longer a stranger!
For i‘ ve held your hand and made you my friend!
The scent of your skin has become familiar...
as our interests turned out to be similar!

By LIS


Be blesses and stay blessed.

L.I.S