Showing posts with label mapenzi. Show all posts
Showing posts with label mapenzi. Show all posts

Thursday, September 1, 2011

Kusaidiana na kupeana moyo....

Behind every successful man is a great woman/Behind every happy woman is a wise man.


Siku zote baba huchukuliwa kama kichwa cha familia na mama ndiye shingo.Shingo inaweza kuelekeza kichwa popote inapotaka, ila ikitokea kichwa kikawa kizito sana itasababisha shingo ielemewe kitu kinachoweza kupelekea shingo kuvunjika.Hivyo hivyo shingo nayo ikiwa lege lege sana inapelekea kichwa kuanguka.


Hivyo basi....kina kaka/baba wasaidieni kina mama kwenye majukumu yao mnayoyaita ni ya wamama ili wasizidiwe sana.Enzi za kusema kulea watoto na shughuli za nyumbani ni za mama tu zimepitwa na wakati.Usiwe mzigo wa kumfanya mwanamke ajutie kukufahamu au aishie tu kuona wenzake wakifurahia maisha, msaidie mwenzako ili mwisho wa siku awe na nguvu za kukusaidia na wewe kwenye majukumu yako.Kusaidiana hakuishii hapo tu....hata kitu kama kupunguza pombe na kumsikiliza/kufuata ushauri wake iwapo una tija ni kumsaidia pia.


Kwa kina dada....wazungu husema ''Behind every successful man is a great woman'' choose to be that woman!Maana sisi kama wanawake(shingo) tuna nafasi kubwa sana katika maamuzi yanayopelekea mafanikio au maanguko ya wanaume.Kumkejeli mwenzako kwa maneno kama ''we ni mwanaume suruali'' ''huna maana '' na mengine kama hayo haifai.Kama angekua hayo yote usingekua naye!Mpe moyo linapokuja swala la kujiendeleza na kwenye maisha yote kwa ujumla...kumkatisha moyo kwa maneno kama '' huwezi kumfikia fulani...ana pesa sana yule'' ''kazi yenyewe unayofanya hata hailipi vizuri'' n.k kutampunguzia kujiamini.Katika watu wote wewe (kama mke, dada, rafiki, mpenzi, mwenzi, mama yake n.k) ndo unatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kumpa moyo na kumuaminisha anaweza na sio kumponda alafu unabaki kushangaa mbona  fulani ana mafanikio zaidi ya huyu wa kwangu wakati hawakua mbali sana.


Mwisho....furaha ya kila mmoja wenu inamtegemea mwenzake kwahiyo heshima iwepo(kupeana na kulindiana)..mapenzi ya dumishwe..kusameheana na kuombana samahani kupewe kipaumbele.. kusifiana na kukosoana kistaarabu nako kusikosekane!!All in all usimtendee mwenzako usiyopenda kutendewa(furahisha kufurahishwa...heshimu kueshimiwa.)


Be blessed ...and stay blessed!
L.I.S

Thursday, August 25, 2011

Dondoo za mapenzi...



Mahsusi kwa watu wanaotarajia kuanzisha mahusiano thabiti na yenye malengo pamoja na wale ambao tayari wamo ndani ya mahusiano ya aina hiyo.

KWA WATARAJIA

1.Usidanganyike na muonekano wa nje au yale maongezi ya mwanzo.
Kila mtu hua mstaarabu siku za mwanzo hata wale ambao sio.

2.Usikimbilie kutangaza nia haraka.
Siku zote ni rahisi mtu kua muwazi kwa rafiki yake kuliko kwa mtu ambae anajua anataka mahusiano nae kwa hofu ya kumpoteza.Tumieni muda wakutosha kufahamiana kama marafiki kabla hamjajiingiza kwenye uhusiano wa kimapenzi.

3.Uliza maswali kuhusu vitu ambavyo ni muhimu sana kwako.
Kwa mfano kama ni mtu wa familia au sio taka kujua mawazo yake kuhusu watoto hii itaepusha migongano isiyo ya lazima hapo baadae.

4.Penda kujua malengo yake ya baadae.
Hii itakuwezesha kugundua ni mtu wa aina gani...kama ni mpenda maendeleo,mtu wa starehe tu n.k.

5.Kua muwazi.
Hii inakwenda kwa pande zote...kuna vitu ambavyo ukimwambia mtu ni vidogo sana ila ukificha vinakua kwa vile tu ulifanya siri.

6.Hakikisha uwezo wenu wa kuelewa unaendana.
Hapa siongelei darasa ila mnavyokua sambamba kwenye maongezi ya kawaida tu yasiyo hitaji degree.

Mimi na wewe....

Siku kadhaa zilizopita nilikua nafikiria kitu nikajikuta naangalia mahusiano na ndoa kwa namna ambayo sikuwahi kabla. Mimi na wewe ni kama vipande vya puzzle ....you've got your share and I have got mine.Ukiviweka pamoja either unapata picha/umbo kamili ama hupati.




Kila mmoja ana shape na size tofauti.Inapotokea wewe kama puzzle umemchagua mtu ambae yeye kama puzzle hana shape zinazoendana na vipande ulivyonavyo ndipo matatizo na migongano inapoanza.Utajitahidi kunoa na kuongeza zile sehemu zisizofit vizuri kwako au kwake ila mwishoni unashangaa pamoja na jitihada zako zile sehemu zinapwaya na ukiendelea kulazimisha zinavunjika na kuvunjika.

So jambo la muhimu hapa ni kutafuta vile vipande ambavyo vinaendana na vyako.One that is complementary to yours....one that accomodates your needs.

Linapokuja swala la ndoa ndo kabisa umakini wa hali ya juu unahitajika.Hapa kinachofanyika ni kuvishikanisha vipande vyako na vya mwenzako kwa glue.Hata kama haviendani at first havitakua na jeuri juu ya glue....ila baada ya muda utashangaa huku kunameguka...na vikianguka tu vinavunjika vunjika.Ila kama vitakua vinaendana ni rahisi kustahimili mitikisiko na mianguko.Hata sehemu ikimeguka ni rahisi kuirudishia.Kwahiyo kuweni waangalifu....usichukue tu vipande ni vipande...

....bali tafuta vile vinavyokufaa!!

Kwa kuongezea.....

Wakati mwingine hutokea kwamba baadhi ya watu wanaona puzzle zao zinafit na baadae hazifit na wengine wanaoona hazifit na baadae wanashangaa sio kama ni miujiza au bahati mbaya vinakua vimewatokea.Bali hayo ni matokeo ya kutumia puzzle za MATAKWA yao kutafuta kile WANACHOHITAJI!!!

Kwahiyo wale wanaopata zinazofit wanakua wamepata kile wanachokitaka...ila baada ya muda mabadiliko yanakuja!Wanagundua kwamba walichotaka na kukipata sicho wanachohitaji!Hivyo hivyo kwa wale wanaodhani wamebahatika kuona muujiza mbele ya macho yao...mtu anakua ametumia puzzle za matakwa na kuona kwamba haziendani na za mwenzake.Ila kumbe zinaendana na mahitaji yake ambayo ni muhimu kuliko matakwa.

Na tatizo hapa ni kwamba wengi hua tunafikiria na kujua ni nini tunachotaka bila kujishughulisha kufahamu tunayohitaji!!!Ndio maana unakuta mtu aliwahi kukupa sifa za atakae kua mke wake baadae ila siku ikifika akakutambulisha unajiliza kama amesahau sifa zake zile au la!Sio kama anakua hajawaona wenye sifa alizotaka awali. Na wakati mwingine unakuta mtu anatamba sana mwanzoni kwamba mwenzangu ana kila NNACHOTAKA ila muda sio mrefu unashangaa akisema yule hakua size yangu au hakunifaa!Ukiangalia sifa zote alizotoa mwanzo kama ni uzuri/pesa/ndoa/ n.k bado viko pale pale!!

Be blessed...and stay blessed.
L.I.S