Showing posts with label malkiasun. Show all posts
Showing posts with label malkiasun. Show all posts

Friday, October 28, 2011

Zawadi sehemu ya 7

Poleni kwa kusubiria sana mwendelezo.....

Kwa dakika nilitamani ningekua na uwezo wa kusoma mawazo ya baba nikajua nini kilikua kinaendelea kichwani kwake .Maana aliyofanya pale wodini yalikua nje ya matarajio yangu kabisa na hata nilipojaribu kufikiria nini kilichosabisha kile nilichoshuhudia sikufanikiwa. Nilidhani labda amechanganyikiwa, lakini hakuonekana kama mtu aliyechanganyikiwa bali mtu mwenye hasira zisizodhibitika.

Pamoja na kwamba baba hakusema neno baada ya zile purukushani hasira zake haziokuonekana kupungua. Wale waliomshika walimuomba watoke nje kidogo nae hakukataa. Akanitazama kwa jicho kali kisha akaongozana nao na kutoka nje ya wodi tuliyokuwamo. Kitendo cha kubaki pale chumbani mwenyewe hakikunipa unafuu bali kilinifanya niogope kile kilichokua kikiendelea. Nilitamani mtu mwingine aje mle ndani ili nijuzwe kilichokua kinaendelea ila haikua hivyo. Mawazo ya kuchomoa dripu niliyokua nimechomekewa mkononi mwenyewe ili nitoke nje yalinijia ila sikuthubutu.

Wednesday, October 19, 2011

Ukishikwa.....

........shikamana!


Inashangaza kweli wakati mwingine jinsi watu wanavyoBEHAVE kwenye mahusiano.Wengine utakuta wanaendekeza KIBURI...wengine KUDEKA...wengine KULALAMIKA...KUGOMBA kila saa n.k tena bila sababu ya msingi.

Vyote hivi vikizidi kwakweli vinaweza kuvunja mahusiano maana INABOA/CHOSHA...kuna mtu unakuta hata akikosea yeye samahani mwiko.Hata ukimuwia mpole japo ye ndo mwenye kosa inakua bado haitoshi....yani kiburi chake ndo kinamtawala.
Wale walalamikaji nao yani utadhani ulimwengu mzima kabebeshwa yeye....kila saa kama anataka kulia..kila kitu ye ni kama anaonewa.Hata akifanya kosa kulia atalia yeye ...na kubembelezwa atabembelezwa yeye.Hawa wadekaji maarufu ndo kabisaaa...mtu kadri unavyombembeleza ndivyo anavyozidisha!Yani utadhani mashindano...mpaka mwisho wa siku mtu unaamua kumpotezea tu!

Nnachosema ni kwamba...mapenzi sio kukomoana jamani!Kila kitu fanya kwa kiasi!Wapenzi/wenza hawatakiwi kua na ushindani...labda kama mnashindana kuonyeshana mapenzi na sio nani kinara wa kulalamika au nani mwenye kiburi zaidi ya mwenzie!Hivyo basi ukishikwa shikamana...ukielezwa elewa...ukipendwa pendeka...ukiheshimiwa heshimu na heshimika pia!

Be blessed and stay blessed!
L..I.S

Monday, August 29, 2011

Zawadi sehemu ya nne....


Sehemu ya nne.........

Siku iliyofuata tulichelewa kuamka kutokana na uchovu wa hadithi za usiku mzima. Aliyetuamsha alikua Jerry aliyetumwa na mama yake kutukaribisha kifungua kinywa. Aligonga mara mbili kabla ya kufungua mlango na kuingia ndani kwa kunyata, pamoja na kwamba tulimsikia wote tulifumba macho kama vile bado tumelala. Alienda moja kwa moja dirishani na kusogeza pembeni mapazia yaliyokua yakizuia jua lililokua linawaka asubuhi ile lisiingie chumbani . Mwanga wa jua ulimmulika Ester aliyekua amelala karibu na dirisha na kumfanya amfokee Jerry kumwomba arudishe mapazia kama alivyoyakuta. “Amka huko acha uvivu. Alafu we ni muongo kweli, jana siuliniambia Zawadi haji wewe?!“ aliuliza Jerry. “Embu ondoka bwana!Au nimwambie mama unatusumbua...!MAMAA!!“ yalikua majibu ya Ester ambae kwa wakati ule hakua tayari kuamka. “Mama mwenyewe ndio kanituma niwaamshe kwahiyo sitoki wala nini.“ nilishawazoea kwa vile ambavyo walikua wakichokozana mara kwa mara, haikua ajabu sababu umri wao haukuzidiana sana hivyo kila mmoja alitaka kumwonyesha mwenzake kwamba hawezi kumtawala.

Thursday, August 25, 2011

Mimi na wewe....

Siku kadhaa zilizopita nilikua nafikiria kitu nikajikuta naangalia mahusiano na ndoa kwa namna ambayo sikuwahi kabla. Mimi na wewe ni kama vipande vya puzzle ....you've got your share and I have got mine.Ukiviweka pamoja either unapata picha/umbo kamili ama hupati.




Kila mmoja ana shape na size tofauti.Inapotokea wewe kama puzzle umemchagua mtu ambae yeye kama puzzle hana shape zinazoendana na vipande ulivyonavyo ndipo matatizo na migongano inapoanza.Utajitahidi kunoa na kuongeza zile sehemu zisizofit vizuri kwako au kwake ila mwishoni unashangaa pamoja na jitihada zako zile sehemu zinapwaya na ukiendelea kulazimisha zinavunjika na kuvunjika.

So jambo la muhimu hapa ni kutafuta vile vipande ambavyo vinaendana na vyako.One that is complementary to yours....one that accomodates your needs.

Linapokuja swala la ndoa ndo kabisa umakini wa hali ya juu unahitajika.Hapa kinachofanyika ni kuvishikanisha vipande vyako na vya mwenzako kwa glue.Hata kama haviendani at first havitakua na jeuri juu ya glue....ila baada ya muda utashangaa huku kunameguka...na vikianguka tu vinavunjika vunjika.Ila kama vitakua vinaendana ni rahisi kustahimili mitikisiko na mianguko.Hata sehemu ikimeguka ni rahisi kuirudishia.Kwahiyo kuweni waangalifu....usichukue tu vipande ni vipande...

....bali tafuta vile vinavyokufaa!!

Kwa kuongezea.....

Wakati mwingine hutokea kwamba baadhi ya watu wanaona puzzle zao zinafit na baadae hazifit na wengine wanaoona hazifit na baadae wanashangaa sio kama ni miujiza au bahati mbaya vinakua vimewatokea.Bali hayo ni matokeo ya kutumia puzzle za MATAKWA yao kutafuta kile WANACHOHITAJI!!!

Kwahiyo wale wanaopata zinazofit wanakua wamepata kile wanachokitaka...ila baada ya muda mabadiliko yanakuja!Wanagundua kwamba walichotaka na kukipata sicho wanachohitaji!Hivyo hivyo kwa wale wanaodhani wamebahatika kuona muujiza mbele ya macho yao...mtu anakua ametumia puzzle za matakwa na kuona kwamba haziendani na za mwenzake.Ila kumbe zinaendana na mahitaji yake ambayo ni muhimu kuliko matakwa.

Na tatizo hapa ni kwamba wengi hua tunafikiria na kujua ni nini tunachotaka bila kujishughulisha kufahamu tunayohitaji!!!Ndio maana unakuta mtu aliwahi kukupa sifa za atakae kua mke wake baadae ila siku ikifika akakutambulisha unajiliza kama amesahau sifa zake zile au la!Sio kama anakua hajawaona wenye sifa alizotaka awali. Na wakati mwingine unakuta mtu anatamba sana mwanzoni kwamba mwenzangu ana kila NNACHOTAKA ila muda sio mrefu unashangaa akisema yule hakua size yangu au hakunifaa!Ukiangalia sifa zote alizotoa mwanzo kama ni uzuri/pesa/ndoa/ n.k bado viko pale pale!!

Be blessed...and stay blessed.
L.I.S

Wednesday, August 24, 2011

What are dreams for...?


To be dreamt and then forgotten...
or remembered but then forsaken?!
I ask for I don't know....
whether to hold on to them or let them go.

Your face so visible and clear...
your voice so sweet to hear!
As real as it may seem ....
it only happens in my dreams.

The way I remember you so clearly..
Ohh how your presence felt so lovely!
I wish I could relive the past....
and make the good days last.

By LIS

Be blessed...and stay blessed.
L.I.S