Monday, August 29, 2011

Tamaa ni mbaya....




Hi guys!

I was inspired to write this article by a friend so a lot of thanks to her.

Na hii ni maalumu kwa wasichana wenzangu!!

Kutoka kwa msichana mmoja kwenda kwa mwingine naanza kwa kusema TAMAA NI MBAYA.

Hivyo usitamani vile vitu ambavyo huna uwezo navyo kiasi cha kua tayari kuomba omba ama kukubali kipatiwa na mtu hata usiyemfahamu. Mara kadhaa nimewahi kusikia baadhi ya wasichana wakiwa reffered kama “ahh yule wa chips mayai tu“ na mwanaume kwasababu yeye tamaa yake ndipo inapoanzia.Kwenye vitu vya kula...kwanzia soda, chips, kuku, pipi pipi na biskuti n.k.Baada ya hapo tunahamia kwenye mavazi, mitoko, namna ya kuishi na kuendelea.Kwa ujumla naongelea vile vitu ambavyo binti anaona fulani anacho au anapata kutoka kwao wakati yeye uwezo huo hana.Hivyo anakua tayari kwa lolote ili naye apate hicho kitu.

Ukweli ni kwamba kwa kuwa na tabia za kuomba omba ama kukubali kupewa vile unavyotamani toka kwa mwanaume unakua unarahisisha wewe kutumiwa kwa namna yoyote ile.

Mwenyewe unaweza ukaona hamna tatizo lolote ikiwa na wewe unamtumia ila jiulize hivi...siku ukikutana na ambae atakutumia bila wewe kutarajia/kutaka ama kupenda kwa mfano KUKUBAKA ama tu ukalazimika kuwa katika mahusiano na mtu ambae pengine ni mgonjwa ukaambukizwa je utajisikiaje?! Probably not good. Alafu ukiachia mbali hisia zako unajua madhara ambayo unaweza ukapata kutokana na hicho kitendo?! Kuna magonjwa ya zinaa..mimba ambayo hukutarajia tena ya mtu ambae hukuchagua kushiriki nae mapenzi..kuathirika kisaikolojia n.k

Hasara ni nyingi hivyo jaribu/jifunze/jitahidi kushinda tamaa zako. Kama wewe mwenyewe huwezi kununua chips kuku au jeans unayoipenda kwa pesa yako mwenyewe au ya kupewa na watu wako wa karibu (ndugu..jamaa na marafiki) achana nayo. Hivi vitu havikimbii...hata baada ya miaka ishirini bado vitakuwepo tu.Kwahiyo tumia muda wako mwingi kujituma shuleni/chuoni kama bado unasoma au kazi kama unayo ili upate mafanikio ambayo yatakuwezesha kujiridhisha wewe na nafsi yako bila kulazimika kumtegemea mtu mwingine.

Kumbuka...hamna bure ambayo ni bure.Kile unachodhani ni bure ni ghali kuliko vile unavyoviona ni ghali .Kwasababu gharama yake huioni hivyo hupati nafasi ya kuamua kama hiyo gharama ina thamani sawa na kile ambacho unaweza ukalazimika kukitoa baadae kama malipo.

TAFAKARI.....JITUME!!!


Be blessed ....and stay blessed!
LI.S

2 comments:

  1. Natumai wamekusikia!!

    ReplyDelete
  2. LIS, thanks for writing this. naomba ruhusa ya kunakili kwa ajili ya wapwa zangu.
    wakati wmingine sio kama wasichana hawana hela ya kujinunulia hizo chips,ni tabia tu ya kupenda mteremko. na ugonjwa umewapata hata wakaka! lets go back to the roots, rape will destroy ur future!
    asante tena kwa kazi nzuri,always!

    ReplyDelete