Sunday, November 27, 2011

Nini maana ya kusamehe. . . ?

Ni nini maana halisi ya kusamehe??
Je ukimsamehe mtu unalazimika kuwa karibu yake tena?? Kurudiana kimapenzi kama ndivyo mlivyokua mwanzo?? Kuongea mara kwa mara kama ndivyo mlivyokua mwanzo? Kutembeleana mara kwa mara kama ndivyo mlivyofanya mwanzo??

Nauliza kwasababu mara nyingi nimeona/sikia watu wakisema ''mi nilidhani umenisamehe/umemsamehe'' pale wanapotaka mambo yarudi kama mwanzo/au hata yawe zaidi na kuambiwa kwamba haiwezekani. Ina maana ukimsamehe mtu moja kwa moja unategemewa/una jukumu la kumchukulia/treat kama vile hilo kosa alilofanya halikuwahi kutokea?

Binafsi naamini kwamba kumsamehe mtu ni kile kitendo cha kuachilia (letting go) kile kilichotokea. Kumruhusu awe na amani..na kufungua ukurasa mpya ambao unaweza ukachagua awepo ndani yake au asiwepo na sio kukifuta kabisa alichofanya na kulazimika kurudi mlipokua mwanzo bila mhusika (mkosewaji) kutaka/penda kufanya hivyo. Yani inawezekana kumsamehe rafiki mwizi bila kumkaribisha tena nyumbani kwako...kumsamehe mke/mume/mpenzi cheater bila kurudiana nae tena..kumsamehe ndugu/rafiki mmbea bila kumshirikisha mambo yako tena. I don't know...inawezekana kwa kufanya hivyo mtu anakua hajasamehe ila ndivyo nnavyoamini na kufanya pia...hata mimi siwezi lazimisha/taka/tegemea mtu niliyemkosea na akanisamehe kurudisha mahusiano yetu ya mwanzo kwasababu tu ameniambia ''NIMEKUSAMEHE''.Ntategemea anipotezee/awe karibu na mimi kwasababu anapenda/taka kufanya hivyo na sio kama jukumu linalofuatana na msamaha wake.


Nilipost hii mada JF wiki kadhaa zilizopita tukawa na majadiliano mazuri kweli . . . tembelea hii link kufuatilia mjadala http://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/195263-nini-maana-ya-kusamehe

No comments:

Post a Comment