Sunday, November 27, 2011

Utegemezi. . . .

Utakuwaje tegemezi?

1.Kwa kukosa maarifa na msukumo wa kujituma. . .
Unakuta mtu hajasoma hivyo inakua ngumu kupata kazi inayorequire kisomo. . . zile za kawaida na ujasirimali anapuuza maana hapendi kujituma.
2.Malezi na mazoea. . .
Kuna watu katika kulelewa kwao walizoe kila kitu kinatoka kwa baba/mama mpaka umri ambao ni mkubwa sana.Yani wanaendekezwa. . . sasa ikitokea yule mzazi hayupo tena au hana uwezo wa kumpa mahitaji yake mtoto (ambae ni mtu mzima sasa) anatafuta pengine pa kutegemea maana hakufunzwa kujitegemea.Watu hua wananyanyasika kweli kwa hii hali. . . ndio maana ni muhimu kuwafundisha watoto kujitegemea kihisia. . . kimatendo na kimawazo.
3.Kutokujiamini. . .
Hii inaweza kuzaliwa namba mbili hapo juu. . . au ikawa tuni matokeo ya low-self esteem and morale.
4.And then there is the Dependent Personality Disorder. . .
Unakuta mtu yeye kama yeye haamini kwamba anaweza kujitosheleza mwenye (emotionally. . financially. . .au hata kimawazo) Yani lazima ategemee watu wengine. . . hivyo ndivyo alivyojengeka.

Binafsi naamini kwamba utegemezi ni ugonjwa mbaya zaidi ya ukoma. . . mbaya zaidi kwa kuwa tegemezi ni sawa na kujiweka mahabusu.Unakosa uhuru wa kufanya yale unayopenda na kuamini. . . unakosa kuheshimiwa. . . unakosa ujasiri wa kusimamia yale unayoona unastahili. . . unashindwa KUWA WEWE na kujikuta unakua yule watu wanaotaka uwe kwasababu unawategemea.

Kama wewe ni tegemezi (hisia zako. . matumizi yako. . .mawazo yako na maisha yako kwa ujumla yanaendeshwa na mtu/watu wengine) anza kuachana na hiyo tabia.
1.Anza kuwa na na mawazo yanayojitegemea.
Usikubali kupelekeshwa na mawazo/imani za watu wengine.Kuwa tofauti na watu wenginesio kosa na wala sio vibaya as long you are not hurting anyone.Let people agree to disagree with you.
2.Jitume.
Kama ni mama wa nyumbani anzisha bustani au kabiashara kako kadogo.Fuga kuku uza mayai. . .nunua mboga mboga za jumla uza mtaani kwako.Yani hakikisha chumvi ikiisha huendi kukopa na kusubiria baba nanii aje umuombe sh.300. Kwa wanaume vile vile. . . yawezekana mkeo ndio mwenye kazi/kipato kikubwa. . . wewe hakikisha tu unatoa mchango wako nyumbani. . . hata kama ni mdogo.
Kama ni binti. . .pangilia pesa ya matumizi unayopewa kama vile umetoka kuifanyia kazi naunaionea uchungu.Jifunze kujipa unayohitaji kabla ya unayotaka kukwepa mitego.
3.Fanya wewe ndio uwe mwamuzi mkuu wa nini kinachoendelea maishani mwako.Kwepa kuwapa watu wengine fursa ya kukuendesha. . . wewe ndo unatakiwa uwe dereva.Ukikata kona unakata kwasababu ndicho ulichotaka na sio ulicholazimika kufanya.

Ila ushauri wangu mkuu unaenda kwa wazazi na walezi ili wadogo zetu nao wasije wakaanguka kwenye dimbwi la kuwa wategemezi.
1.Jitahidi kumpa mwanao/nduguyo elimu ya darasani pia ya maisha.Akifaulu yote atakua na mafanikio kimaisha na kiakili.
2.Mruhusu/mfundishe kujieleza pale mnapokua mmepishana badala ya kusema tu "wewe ndie mwamuzi". . . hata kama ni kweli reason with him/her ili aelewe kwanini.Hii itamsaidia kuwa na mawazo yanayojitegemea badala ya kuwa bendera fuata upepo.
3.Mfundishe kusimamia kile anachoamini as long as hatendi kosa.
4.Mfundishe kujituma. . .mpe kazi ndogo ndogo hata kama mna mfanyakazi/ wafanyakazi.
5.Mjengee kujiamini.
6.Hii inashirikiana na namba nne na ntaitolea mfano.Mfundishe THAMANI YA PESA.Ndio inawezekana uwezo unao wa kumnunulia kila atakacho ila kwa kufanya hivyo hutokua unamsaidia maana mbeleni hayo mazoea yatakuja kumsumbua.

Mfano. . .badala ya kutengewa chakula mezani na kuondolewa nvyombo. . .kutandikiwa kitanda na kusafishiwa chumba chakulala anaweza akafanya hizi shughuli mwenyewe. It only takes a couple of minutes a day. . ila somo lake litadumu maisha.Nakumbuka sisi nyumbani tulikua na sheria. . .ukila/kunywa kitu bila watu wengine lazima usuuze vyombo utakavyochafua.Vyombo vyote vilikua vinaoshwa na mtu mmoja baada ya milo ya pamoja tu.
Pesa tulikua tunapewa allowance kila mwezi. . .bila masharti.Ila sasa ilikua mtu ukitaka vitu ambavyo sio neccessities (video games,CDs,sijui music players na vikorokoro vingine vya aina hiyo ) unaulizwa kwanza una sh. ngapi. Tulikua tunatakiwa tusave atleast nusu ya bei ya hicho tunachotaka alafu tuongezewe nusu.Au unakopa na kukatwa kwenye allowance inayofuata.
Hii kitu ilitufanya tuwe tunaheshimu vitu vyetu na kujiuliza mara mbili mbili "do I really need/want this" kabla ya kununua kitu.It helped. . .maana mpaka leo na kesho hua sinunui wala sitaki kitu nisicho na uwezo nacho hata kama nakitamani.
Na mwisho wa siku mtu akiruhusu tamaa imtawale lazima utegemezi umtembelee pale atakapokua hawezi kuridhisha tamaa yake maana kuidhibiti hawezi.


Have a nice weekend.

No comments:

Post a Comment